Jumapili, 1 Januari 2017

SALAMU ZA MWAKA MPYA

SALAMU ZA MWAKA MPYA 2017



GREAT MESSAGE TO THE SOLIDERS OF JESUS CHRIST AND OTHERS
Please read it(Somaaaa itakusaidia sana)
UJUMBE WA MWISHO WA MWAKA 2016 NA MWANZO WA MWAKA 2017
 Yaliyomo
*      MWISHO WA MWAKA
*      Mfano juu ya mtazamo wangu juu ya neno “Mwisho wa mwaka”
*      Mambo ya kufanya ifikapo mwisho wa mwaka Kutokana na mfano huo;
*      Mshukuru Mungu kwa kufika mwisho huu salama haijalishi upo katika hali gani;
*      Kiri/Yaseme mbele za Mungu, kwa kinywa chako yale yote Mungu aliyokutendea.
*      MWANZO WA MWAKA
*      MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOUANZA MWAKA

UTANGULIZI
Mafanikio ya mtu hupimwa pale anapoanza au anapomaliza. Akiwa anaanza (MWANZO) basi hupimwa kwa mikakati yake na maandalizi yake kwajili ya jambo lililopo mbele yake. Mtu akiwa na maandalizi hafifu basi hata mafanikio yake yanakuwa hafifu au anapata hasara kabisa kwa jambo analotaka kulifanya. Hivyo kila mtu  anapaswa awe mwangalifu wa kila mwanzo wa chochote. Na kwa upande mwingine mafanikio ya mtu hupimwa kupitia MWISHO WAKE, mwisho wa kitu chochote ndipo unapima kama mtu amefanikiwa au la! Mikakati yake na mambo aliyotakiwa kuyafanya je amefanikiwa au la! Katika ujumbe huu wa mwanzo wa mwaka 2017. Nitazungumzia mambo machache kila mtu anapaswa kuzingatia kila afikapo mwanzo wa mwaka na mwisho wa mwaka. Barikiwa na ujumbe huu!!  Ni vyema kama utautuma na kwa rafiki zako nao wajifunze mambo haya bado hawajachelewa kufanya kila lililopo humu.



1.    MWISHO WA MWAKA
Mfano juu ya mtazamo wangu juu ya neno “Mwisho wa mwaka”
Mwisho wa mwaka ninaufananisha na Mwanariadha  maarufu awapo uwanjani katika mashindano ya kukimbia ya mita 10,000; ambapo amekimbia muda mrefu, kwa nguvu nyingi akiwa na nia ya kumaliza mbio akiwa mshindi. Ambapo anapo karibia kuufikia mwisho anageuka nyuma na kuangalia kama kuna aliye karibu naye au la! na hapo ndipo anagundua kwamba hakuna aliye karibu naye, huku anaendelea kuufikia mwisho anatafakari wale wote alioanza nao mbio wameelekea wapi. Anaamua kugeuka tena mara hii anawaona wachache tu kwa mbali wanamfuata; hapop teana anajiuliza, Kwanini ni hawa tu wengine wa wapi? Maswali haya anajiuliza japo anatamani kuweka rekodi ya kumaliza akiwa mshindi wa kwanza kwa kuwaacha wenzake umbali mrefu.
Anapoendelea kujiuliza hivyo anashangaa amekwisha maliza umbali wote aliotakiwa kukimbia, na anashangiliwa kwa kumaliza mbio zile kwa nafasi ya kwanza. Anajikuta amemaliza yeye peke yake wa kwanza na wengine wachache wakaja baadae kwa kuchelewa ila wengine walishindwa kabisa kufika. Ndipo hapo anapata majibu kwamba wengine hawakujiandaa vyakutosha hivyo milli yao iliishiwa nguvu na wengine miili yao ili kuwa dhaifu hivyo waliishia katikati pia wengine walikata tamaa baada ya kuona wanapitwa na wenzao.  Kitu kilicho nifurahisha ni baada ya yule mwana  riadha kuona vile alipiga magoti pale pale uwanjani na kumshukuru Mungu.
Mambo ya kufanya ifikapo mwisho wa mwaka Kutokana na mfano huo;
Ni wengi ambao tumeanza nao mwaka 2016 lakini hadi kufikia tarehe 31/12/2016 hatuwaoni, hatupo nao wamefariki. Wengine mili yao imekuwa ni dhaifu na wamelazwa hospitalini. Wengine wameondokeawa na wapendwa wao. Pia wengine wameshindwa kumaliza mwaka wakiwa washindi wa kwanza kama yule mwanariadha, waliweka malengo mengi kwaajili yam waka 2016 kiuchumi, kielimu na kijamii lakini hawajafanikiwa.
Kitu cha Muhimu cha kujiuliza ni kwamba wewe ni nani hata umalize mwaka ukiwa mshindi? Kwanini yale yote uliyoyapanga yamefanikiwa? Je wewe ni bora kuliko wao? Je upo hai kutokana na matendo yako mema? Jibu la maswali haya na mengine mengi  kama haya ni hili “HAPANA”. Sio kwammba wewe ni mwema sana kuliko wengine au ni bora kuliko wengine ila ni KRISTO aliye kustahilisha tu. Kwa neema yake nyingi na ya ajabu.
v  Mshukuru Mungu kwa kufika mwisho huu salama haijalishi upo katika hali gani; umgonjwa au umeondokewa na mpendwa wako. Nimekufananisha na mwana riadha hodari kwasababu ndivyo fikra za mwanadamu zinavyo mdanganya pale anapoona amevuka mwaka wa kwanza, wa pili hadi miaka arobaini kwa ushindi hapo hujisahau na kushindwa kumtukuza Mungu kwa kumfikisha mwaka mwengine. Mwanariadha yule mahiri wa kushindana alipofika mwisho alitafakari na kujiona kwamba sio kwa uwzo wake ila ni kwa neema ya Mungu tu, alipiga magoti na kumtukuza Mungu. Ndivyo unavyopaswa ufanye mpendwa mshukuru Mungu kwa maana ni kwa neema yake kuu amekupa uhai na amekushindia majaeibu mbalimbali uliyopitia.
v  Kiri/Yaseme mbele za Mungu, kwa kinywa chako yale yote Mungu aliyokutendea. Yataje yote unayoyakumbuka makubwa kwa madogo na yale usiyo yakumbuka yataje kwa ujumla wake ukisema neno hili “PAMOJA NA YALE NISIYO YA FAHAMU. Kitendo cha kuyakiri mojamoja kila jambo ambalo Mungu amekutendea kwa kipindi cha mwaka mzima, tabia hii inamfurahisha Mungu na inaonyesha kwamba unathamini yale ambayo MUNGU amekutendea. Mfano wa kutaja ni huu: Na kushukuru Mwenyezi Mungu kwa jinsi ulivyonipigania katika mwaka mzima huu umenipa elimu na umenipandisha kwenye viwango vya juu vya grade A uhimidiwe Bwana. Pia huku nipungukia umenipa kazi nzuri nitakayopata mshahara mzuri……  Huu ndiyo wakati ambao Mungu anatulia na kusikiliza shukrani zako na anajivunia kwa yale yote aliyokutendea. Faida ya kuomba hivi ni hii; 1Unaonyesha unyenyekevu mbele za Mungu hivyo Mungu atakuinua Zaidi katika mwaka mpya. 2Unaonyesha kwamba umethamini kile Mungu alicho kutendea hivyo atatenda Zaidi. 3Mungu atakupa upendeleo wa baadhi ya mambo ambayo yanapaswa yatendewe kazi ili ufalme wake uinuliwe. 4Mungu atakupa hata vile ambavyo huja mwomba. Faida zipo nyingi sana iliyokuu ni kwamba Mungu atakupenda Zaidi na Zaidi na atatamani kukusaidia kila wakati na kukuinua. Soma Zab. 34:7-9, 125:1-2


2.    MWANZO WA MWAKA
MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOUANZA MWAKA
Kuanzia Mita 1 hadi mita 10000 kwenye riadha huu ni umbali wa mwaka mzima: mwaka una miezi kumi na miwili ambapo ni siku 365. Ndani ya mwaka mzima huu kuna kukata tamaa kutokana na yale uliyoyategemea hayajafanikiwa au kile ulicho kipanga hakijafanikiwa au hujajiandaa  vyema.
Kabla ya mwaka haujaisha unapaswa kuzingatia haya: 1Mshukuru Mungu kwa mwaka unaoisha, kama nilivozungumza hapo juu kwamba kufanya hivi kunaushusha uwepo wa Mungu lakini kunamweka Mungu tayari kwaajili ya kukusaidia pindi tu mwaka mpya unapoanza, 2Kamata siku, masaa, dakika, na sekunde katika maombi;  Huku kutakuhakikishia ulinzi muda wowote kwenye ya mwaka unaoanza ukiwa umelala au upo macho Malaika wa Bwana watakuwa na wewe (Zab.34:7).   3Weka mikakati kwaajili ya mwaka  mzima na mshirikishe Mungu mikakati hiyo. Jambo hili litakupa uwezo wa kuwa na nidhamu ya muda na nafasi utakazozipata tokea mwanzo hadi mwisho wa mwaka, hutatamani muda upotee. Pia kumshirikisha Mungu mikakati  yako ni kumshirikisha Mungu maisha yako na Mungu akihusika kwenye maisha yako yote basi ushindi ni lazima. Kila wakati utakapoenda mbele za Mungu katika kipindi cha mwaka mzima ukiwa unaomba kwaajili yako utamkumbusha malengo haya na mengine atakayokuonyesha, Pia utaishi kwa malengo ya kufika sehemu fulani kila iitwapo leo, na malengo yako utafanya juhudi kuyatimiza. 4. Kiri ushindi juu ya mwaka huu mpya, Yoh 1 inatuambia kuhusu Neno kufanyika mwili, ndivyo ilivyo Mungu alitamka kwenye uumbaji ikawa , katika uumbaji wote alisema Maneno haya “NA IWE….” “Ikwa” (Mwa.1). Nasi tuliumbwa kwa mfano wa Mungu hivyo tumepewa uwezo wa kuumba kupitia vinywa vyetu, Neno linasema Uzima na Mauti vipo katika uwezo wa Ulimi. Hii ndivyo ilivyo , ndiyo maana tunaona mzazi anaweza kumlaani mtoto na ikawa. Na si hivyo tuu bali unaweza kujitamkia jambo baya nalo likatokea basi kama ni hivyo unapoingia kwenye mwaka mpya tarehe za kwanza unaanza kuutamkia Baraka na mafanikio mwaka huo juu yako na kwa ndugu zako hata majirani na taifa kwa ujumla.
NAKUTAKIA HERI YA MWAKA MPYA!!!!!!! MWAKA HUU UKAWE WA BARAKA TELE MAISHANI MWAKO NA WENYE MAFANIKIO TELE. AMEN;
BY PRIEST MELCHIZEDEK POKEAELI!!!!!!
(C) Jan.-2016 pokeaeli