Jumatatu, 27 Machi 2023

TAMBUA WAKATI WA KUJILIWA KWAKO. WAKATI WA MUUJIZA WAKO

 Mfano wa Mwanamke wa Sarepta,

Katika wakati huohuo ukiwa na njaa Kali NDIPO Bwana anahitaji umtumikie Kwa uaminifu Ili akuinue. Unapimwa Imani yako kwake. Wakati wa Shibe pia usiache kumtumikia 


Wengine wanadhani kutoa sadaka ni Hadi wawe na utajiri mwingi lakini hapana. Embu angalia kisa hiki.

1 Fal 17:8-16 SUV

Neno la BWANA likamjia, kusema, Ondoka, uende Sarepta, ulio mji wa Sidoni, ukae huko. Tazama, nimemwagiza mwanamke mjane wa huko akulishe. Basi, akaondoka, akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni nipate kunywa. Alipokuwa akienda kuleta, akamwita akasema, Niletee, nakuomba, kipande cha mkate mkononi mwako. Naye akasema, Kama BWANA, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili niingie nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe. Eliya akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye kama ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate mdogo ukaniletee; kisha ujifanyie nafsi yako na mwanao. Kwa kuwa BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Lile pipa la unga halitapunguka, wala ile chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile BWANA atakapoleta mvua juu ya nchi. Basi akaenda, akafanya kama alivyosema Eliya; na yeye mwenyewe, na Eliya, na nyumba yake, wakala siku nyingi. Lile pipa la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la BWANA alilolinena kwa kinywa cha Eliya.

Encouraging and challenging you to seek intimacy with God every day.


YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy.



Jumatano, 2 Novemba 2022

INUKA EWE SHUJAA vol.1

MUNGU ANAKUHITAJI: ENENDA KWA UWEZO ULIO NAO. (Soma Hadi Mwisho hutajuta fuatilia kila siku mwendelezo)


Mungu alipomwita Daudi sio kwamba hakuona kwamba ni Mdogo, au kwamba kwao alikua anadharaulika Ndie wakwenda kuchunga Kondoo za Baba yake. 


Waefeso 3:20-21 SUV

"Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; naam, atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina."


Mungu amepanda nguvu ya ajabu ndani yako ya kuwezesha kutoka katika hali uliyo nayo. Kuvuka ng'ambo nyingine. Nguvu ya kuwezesha kufanya mambo makubwa kwenye maisha yako na ukaleta mabadiliko makubwa kwako, kwa familia na jamii nzima. 


HILA ZA ADUI NA MBINU ZAKE

Adui anachofanya ni kukuambia kwamba huwezi.

Adui anachofanya kingine ni kukuonesha mazingira ya wengine waliothubutu wakashindwa. Anakutengenezea mazingira magumu Ili na wewe ukate tamaa. 


USIKUBALI MAZINGIRA YAKUKWAMISHE

Umaskini usikukwamishe. Kuzaliwa maskini sio makosa yako, makosa yako ni kufa maskini. 


KUA NA UJASIRI KAMA WA DAUDI: KUA NA IMANI THABITI KWA MUNGU WETU.

1 Samweli 17:45

"Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la BWANA wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana." 


Tunalo Jina Lenye Nguvu kupita yote. Kupita Majeshi, Silaha ,Upanga, Njaa Dhiki nk.


INUKA EWE SHUJAA. USISITESITE SONGA MBELE

Ebr 10:38 SUV

"Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye."


Waefeso 3:20-21 SUV

"Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; naam, atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina."

Endelea kufuatilia sehemu inayokuja........


@ Rev.Johnson Pokeaeli

Joyful House In Jesus Christ

Jumatatu, 28 Machi 2022

JIFUNZE LUGHA YA ALAMA NA MADAM IMMAKULATA

 Angalia video hii usisahau kusubscribe


https://youtu.be/fjqM2I29HX4

IF GOD SAYS YES NOBODY CAN SAY NO

 🌅🙏💒 *JOYFUL HOUSE IN CHRIST*🙏💒🌄🌅

*SHALOM JHC*

________________________________

*IN CHRIST JESUS ALL GOD'S PROMISES ARE YES AND AMEN*

________________________

*2 Corinthians 1:20*

New King James Version (NKJV)


*_“For all the promises of God in Him are Yes, and in Him Amen, to the glory of God through us.”_*


What a great promise of God we have today in *2 Corinthians 1:20.* We see that for no matter how many promises God has made, they are “Yes” in Christ. And so through him the “Amen” is spoken by us to the glory of God.


In *Revelation 3:14,* the Lord Jesus is called the “Amen.”  We know that a promise is an oral or written agreement to do or not to do something, and in today’s promise, God tells us that He is dedicated to fulfill ALL His promises, by a Yes and Amen!


What to do from our part? You just need to make sure that your situation is in line with God’s Word, then believe and receive in Jesus name! Can you imagine that there are over 3000 promises of God for us to claim over our life in God’s Word, and to already know each of them is already a “Yes”, and a “Amen”


We serve and worship a faithful God! His word is limitless and all-powerful. We can find a perfect example of the faithfulness of the Word of God. Sarah did not believe for a second the promise of a son, but did God still fulfill it? Yes, Sarah bore Isaac despite of her age! And I just love the way God responded to Sarah in Genesis 18, when she had an unbelief laugh hearing God’s promise of a son, and the Lord answered her: ” Is there anything too hard for THE LORD?” We need to recognize that God is faithful and all-powerful.


All the Abigail, I invite you today to take a look at your life and ask yourself this:


Do I believe God when He said that the plans that He has for me are plans for welfare and not for calamity to give me a future and a hope? (Jeremiah 29:11), and that when He promises, He inevitably executes (2 Corinthians 1:20) or do I just choose to ignore His promise and voluntary live a sinful situation just because I am not able to wait and believe His promise?

I pray for all of us that Jesus who is the Master of our faith to fill us with unwavering faith in Him so we can embrace the life of the new creature that we are as daughters of God.


QUESTION: If you haven’t stand still in God’s promises, what are your plans to do so?


Until then, all the Abigails of God, remember that you are the Joy of God, stay blessed in Christ.


©2022 JHC

Ijumaa, 9 Julai 2021

MAHUSIANO NA MUNGU

 💒JOYFUL HOUSE IN CHRIST💒


🌅MAHUSIANO NA MUNGU🌅


Ni ajabu Ila Ni kweli, hatuwezi kusema tunampenda Mungu Kama tunashindwa kuwapenda wenzetu tunaowaona.


Kristo anatufundisha ,tukitaka kumpenda Mungu hakika tunawajibu wa kuwapenda wenzetu Kama tunavyojipenda wenyewe *Mathayo 22:39* na kuwatendea wengine Kama tunavyopenda kutendewa sisi *Mathayo 7:12*


*Tunawezaje kuwapenda wenzetu?*


1. Kwa kuwahurumia. Katika maisha wenzetu wanapitia shida, mahangaiko kwenye mahusiano, familia ,ndoa. Mm nilie jiran natakiwa kumhurumia na kumsaidia kwa sala, mawazo, faraja na kampani. *Luka 6:36*. Tusiseme muache na akome maana anajidai, hapana. Tunatakiwa tuonyeshe huruma .


2. Kristo anatufundisha tukitaka kuwapenda wenzetu Basi tuwe tunawasamehe. Tuwe na mioyo ya kuwasamehe wenzetu wanapotukosea, na tusiwahukumu au kuwanyima Jambo fulani kisa walitukusea siku fulani. Kristo pamoja na kutendewa mabaya hakika aliendelea kusamehe *Luka 23:34*


3. Tukitaka kuwapenda wenzetu Basi tuwe tunawaombea, sala Ina nguvu. Sala inafika pale ambapo sisi wenyewe kimwili hatuwez fika  . Tuwaombee wenzetu wenye shida, wasio mjua Mungu bado, wanaoishi kwenye dhambi ili Neema ya Mungu iwaguse na wapate kuong'oka na kuishi kadiri ya mapenz ya Mungu.


4. Kristo anatufundisha tukitaka kumfuata lazima tujenge tabia ya kuwa wamisionary, watu wa kuwapelekea Habar Njema wengine. Kwa Karne hii ,njia ya kupeleka Habar Njema imezidi kurahishwa maana Kuna vyombo mbalimbali tunavyoweza kuvitumia kuwafikia wengine hasa mitandao ya kijamii. Tutumie mitandao hii kupeleka Ujumbe wa matumaini, Imani, huruma ,upendo kwa wengine. Tusiishie tu kuweka picha, katuni, bali tuweke ujumbe wa Mungu ili wengi wapate kumjua Mungu.


5. Tukitaka kuwapenda wenzetu basi tuwe tunawasaidia wenzetu wasionacho. Tuweke hata malengo ya kila siku,wiki ,mwezi . Mfano, kila siku nitoe 100, 200, 500 , 1000, chochote nilichobarikiwa nacho kumsaidia asie nacho. Basi hata Kama huna kitu, Basi Neno lako la Faraja latosha kwa mhitaji. 


Mungu atubariki Sana.

@Deusdedith Msungo

©JHC 2021.