Ijumaa, 9 Julai 2021

MAHUSIANO NA MUNGU

 💒JOYFUL HOUSE IN CHRIST💒


🌅MAHUSIANO NA MUNGU🌅


Ni ajabu Ila Ni kweli, hatuwezi kusema tunampenda Mungu Kama tunashindwa kuwapenda wenzetu tunaowaona.


Kristo anatufundisha ,tukitaka kumpenda Mungu hakika tunawajibu wa kuwapenda wenzetu Kama tunavyojipenda wenyewe *Mathayo 22:39* na kuwatendea wengine Kama tunavyopenda kutendewa sisi *Mathayo 7:12*


*Tunawezaje kuwapenda wenzetu?*


1. Kwa kuwahurumia. Katika maisha wenzetu wanapitia shida, mahangaiko kwenye mahusiano, familia ,ndoa. Mm nilie jiran natakiwa kumhurumia na kumsaidia kwa sala, mawazo, faraja na kampani. *Luka 6:36*. Tusiseme muache na akome maana anajidai, hapana. Tunatakiwa tuonyeshe huruma .


2. Kristo anatufundisha tukitaka kuwapenda wenzetu Basi tuwe tunawasamehe. Tuwe na mioyo ya kuwasamehe wenzetu wanapotukosea, na tusiwahukumu au kuwanyima Jambo fulani kisa walitukusea siku fulani. Kristo pamoja na kutendewa mabaya hakika aliendelea kusamehe *Luka 23:34*


3. Tukitaka kuwapenda wenzetu Basi tuwe tunawaombea, sala Ina nguvu. Sala inafika pale ambapo sisi wenyewe kimwili hatuwez fika  . Tuwaombee wenzetu wenye shida, wasio mjua Mungu bado, wanaoishi kwenye dhambi ili Neema ya Mungu iwaguse na wapate kuong'oka na kuishi kadiri ya mapenz ya Mungu.


4. Kristo anatufundisha tukitaka kumfuata lazima tujenge tabia ya kuwa wamisionary, watu wa kuwapelekea Habar Njema wengine. Kwa Karne hii ,njia ya kupeleka Habar Njema imezidi kurahishwa maana Kuna vyombo mbalimbali tunavyoweza kuvitumia kuwafikia wengine hasa mitandao ya kijamii. Tutumie mitandao hii kupeleka Ujumbe wa matumaini, Imani, huruma ,upendo kwa wengine. Tusiishie tu kuweka picha, katuni, bali tuweke ujumbe wa Mungu ili wengi wapate kumjua Mungu.


5. Tukitaka kuwapenda wenzetu basi tuwe tunawasaidia wenzetu wasionacho. Tuweke hata malengo ya kila siku,wiki ,mwezi . Mfano, kila siku nitoe 100, 200, 500 , 1000, chochote nilichobarikiwa nacho kumsaidia asie nacho. Basi hata Kama huna kitu, Basi Neno lako la Faraja latosha kwa mhitaji. 


Mungu atubariki Sana.

@Deusdedith Msungo

©JHC 2021.

EVENING GLORY

 ⛪ *JOYFUL HOUSE IN CHRIST*⛪


*EVENING GLORY*

09/07/2021.

-------------------------

 *Mithali 16:9*

*9 Moyo wa mtu huifikiri njia yake;  Bali Bwana huziongoza hatua zake.*


*TAFAKARI FUPI*

Sasa tuko MUHULA wa pili kukamilisha mwaka nikimaanisha tuko mwezi wa Saba sasa. *Unaendeleaje na mabadiliko hayo na ahadi ulizotoa kwa mwaka 2021?*

*Ni kwa viwango gani hiyo mipango yako imekamilika.?*

Ila  Usikate tamaa au kuyaacha  hayo malengo... hata ikiwa kuna shida na changamoto ya kukaa kwenye mstari kutimiza malengo yako . Lakini, hebu  tukumbuke kwamba BWANA ndiye Aziongozae njia zetu, mwisho wa mawazo yetu ndio mwanzo wa njia zake, na Biblia inatueleza kuwa *Yeye anautangaza mwisho tokea mwanzo* hivyo yeye alishajua hatima ya malengo yako tokea Mwanzoni mwa mwaka huu,hivyo 

Nishauku yangu kuona  tunabaki ndani ya kusudi la Mungu, na kumuuliza Bwana Ni wapi anataka tuende na kile anataka tufanye, kisha tuende huko na tufanye.


Then *utakusudia Jambo nalo litathibitika kwako* 


*TUOMBE*

Mungu Mtakatifu, Bwana Mwenyezi, Abba yaan Baba, asante kwa kuwa Ni wa  kushangaza, mtakatifu, na mwenye nguvu. Asante pia kwa kujali kutujali , maisha yetu, maamuzi yetu, na mapambano yetu. Tunaomba tuongoze kwa Roho wako ili tuweze kuelewa Neno lako na kutambua mapenzi yako kwa maisha yetu.ili tukazidi kukuelekezea kikamilifu hatua zetu. Kwa jina la Yesu Kristo ninaomba na kuamini . AMINA


*Nikutakie jioni njema na usiku mwema mpendwa*


*@Dr Mwanga*


*Thus far as God helped us*


*@2021 Joyful house in Christ*

Alhamisi, 8 Julai 2021

MORNING GLORY

 ⛪⛪ *JOYFUL HOUSE IN CHRIST* ⛪

   *MORNING GLORY*

Tar. 09/07/2021.

--------------------------

*Mithali 10:11*

*11 Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima;  Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,*

 

=>Ukitaka kujua tofauti kati ya mtu mwadilifu na mtu mwovu? Rahisi, angalia matunda ya maisha yao. Moja ya aina ya matunda inayoonekana katika maisha ya mtu ni *hotuba yake*. Mtu mwadilifu huongea maneno ya hekima, mazuri ambayo ndani yake Kuna *faraja*, uponyaji na Zaidi ya yote uzima 

 *Zekaria 1:13*

*"Naye BWANA akamjibu yule malaika aliyesema nami kwa maneno mazuri, maneno yenye* *faraja.* "

Biblia inasema Wafalme kutoka nchi mbalimbali walimuendea mfalme Sulemani ili kusikiliza Hekima yake. Hii inaonyesha ndani ya hekima ya *Sulemani* walipata suluhisho la changamoto wanazokutana nazo ,na pengine walipata hata miongozo kadhaa ya namna ya kuoongoza nchi zao, Nani anajua! 

Bali Waovu watajidhihirisha kila wakati kwa kile kinywa chake kinasema.kwa sababu ndicho kilichomjaza moyo wake. Mungu ana maana kubwa kutuonya tusikae barazani pa wenye mizaha, tafsiri yake Ni kwamba  hutapata hekima Bali mizaha tu na jeuri. Na mwisho utaishia KUTENDA dhambi.

Zaidi ya yote Mungu anatupenda Sana na ndio maana leo anatukumbusha *1Timotheo 4 :12*

 *Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi* 

=> Ni ombi langu Asubuhi ya Leo ukawe na usemi mzuri wenye Hekima ndani yake ili mtu awaye yote asikudharau daima.


*TUOMBE*

*Tunakushukuru Mungu kwa namna ulivyotuamsha wenye nguvu na afya tele  na kutupa tafakari hii fupi ya neno lako kwa Asubuhi hii  ya leo tunaomba  Maneno ya Vinywa vyetu na tafakari za mioyo yetu na zipendeze mbele zako, Ee Mungu Baba yetu,  mkombozi, na BWANA Wetu ili tukawe vielelezo Bora kwa wale watuzungukao  Sasa na hata milele. Kwa jina la Yesu Kristo Nimeomba na kuamini  Amina.*


Uwe na siku njema!!


@ *Dr Mwanga.*

*Thus far as God helped us*


*@2021 JOYFUL HOUSE IN CHRIST*