⛪ *JOYFUL HOUSE IN CHRIST*⛪
*EVENING GLORY*
09/07/2021.
-------------------------
*Mithali 16:9*
*9 Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali Bwana huziongoza hatua zake.*
*TAFAKARI FUPI*
Sasa tuko MUHULA wa pili kukamilisha mwaka nikimaanisha tuko mwezi wa Saba sasa. *Unaendeleaje na mabadiliko hayo na ahadi ulizotoa kwa mwaka 2021?*
*Ni kwa viwango gani hiyo mipango yako imekamilika.?*
Ila Usikate tamaa au kuyaacha hayo malengo... hata ikiwa kuna shida na changamoto ya kukaa kwenye mstari kutimiza malengo yako . Lakini, hebu tukumbuke kwamba BWANA ndiye Aziongozae njia zetu, mwisho wa mawazo yetu ndio mwanzo wa njia zake, na Biblia inatueleza kuwa *Yeye anautangaza mwisho tokea mwanzo* hivyo yeye alishajua hatima ya malengo yako tokea Mwanzoni mwa mwaka huu,hivyo
Nishauku yangu kuona tunabaki ndani ya kusudi la Mungu, na kumuuliza Bwana Ni wapi anataka tuende na kile anataka tufanye, kisha tuende huko na tufanye.
Then *utakusudia Jambo nalo litathibitika kwako*
*TUOMBE*
Mungu Mtakatifu, Bwana Mwenyezi, Abba yaan Baba, asante kwa kuwa Ni wa kushangaza, mtakatifu, na mwenye nguvu. Asante pia kwa kujali kutujali , maisha yetu, maamuzi yetu, na mapambano yetu. Tunaomba tuongoze kwa Roho wako ili tuweze kuelewa Neno lako na kutambua mapenzi yako kwa maisha yetu.ili tukazidi kukuelekezea kikamilifu hatua zetu. Kwa jina la Yesu Kristo ninaomba na kuamini . AMINA
*Nikutakie jioni njema na usiku mwema mpendwa*
*@Dr Mwanga*
*Thus far as God helped us*
*@2021 Joyful house in Christ*
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni