Alhamisi, 25 Mei 2023

UTAJIRI NI HAKI YAKO, UPO MIKONONI MWAKO

 MAISHA MAZURI NI HAKI YA KILA ALIYEUMBWA NA MUNGU

✍️Rev. Johnson Paul Pokeaeli



MAMBO MAWILI MUHIMU

1. Mungu alimwumba Binadamu siku ya sita baada yakumwandalia kila kitu. Chakula, mahali pazuri pakuishi, mazingira salama nk. Soma Mwanzo 1.

2. Mungu alimpa Mwanadamu maarifa ya kuvitumia, na mamlaka Ya kuvitumia na wajibu wa kuvitunza

UUMBAJI SIKU SITA MAANDALIZI KWAAJILI YA MAISHA MAZURI YA MWANADAMU

Siku ya 1: Mungu aliumba nuru iangaze uso wa dunia na kuwezesha kuwa vipindi vya usiku na mchana.—Mwanzo 1:3-5.

Anga na bahari

 Siku ya 2: Mungu aliumba anga, au alitenganisha maji yaliyo chini ya anga na maji yaliyo juu ya anga.—Mwanzo 1:6-8

Nchi kavu na mimea

 Siku ya 3: Mungu alitokeza nchi kavu. Aliumba pia mimea.—Mwanzo 1:9-13

 Siku ya 5: Mungu aliumba viumbe wa kwenye maji na wanaoruka.—Mwanzo 1:20-23

Siku ya 6: Mungu aliumba wanyama na wanadamu.—Mwanzo 1:24-31. .31.

TAMBUA THAMANI YA DUNIA MUNGU ALIYOKUPA

-uhai ni Fursa Kubwa sana kufanya badiliko katika ulimwengu wa Roho na wa MWILI.

•Mungu alipomwumba Mwanadamu alipomaliza alimpulizia Pumzi hai akawa kiumbe hai.

°ungali unaishi bado una nafasi ya kufanya Jambo chanya kwaajili ya maisha yako ya sasa na hata ya baadae.

°TOBA NA MAISHA SAFI -Inakupa uhakika wa maisha mazuri ya Sasa hata ya baadae

*BIDII BINAFSI - Inakupa nafasi ya kupata Chakula Cha Kila siku.



HIVYO VYOTE MUNGU ALIUMBA SIKU SITA KWAAJILI YAKO MWANADAMU.

WEWE NI WATHAMANI MNO.

MTUKUZE MUNGU

MUNGU HAKUUMBA GHOROFA/MAGARI/NDEGE AU TRENI.

ILA ALIMPA MWANADAMU MAARIFA

MUNGU AKASEMA, NA tumfanye mtu Kwa mfano wetu akatawale_.

WEWE NA MIMI TUMEUMBWA KWA MFANO WA MUNGU

USIJIDHARAU KWA NAMNA YEYOTE ILE

____________________________________________

Mwanzo 1:26

[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 


And God said, Let us make man in our image, after our likeness: and let

Wewe ni mfano wa Mungu. Ni sura ya Mungu.

Umepewa kutawala kwasababu wewe umeumbwa na Mungu Kwa mfano wake na sura yake.

HIVYO NDANI YAKO KUNA NGUVU YA AJABU AMBAYO HUJAWAI ONA.

•Hujajisumbua kutaka kuona ni nini Mungu ameweka kama hazina ndani yako na ndiyo maana umebaki hivyo ulivyo na hata umekata tamaa kabisa ya kuishi. Soma ✍️*

Efe 3:20-21 SUV

"Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; naam, atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina."


MIKONO ya mwenye BIDII hutajirisha


Dunia ya Sasa inashuhudia watu wengi wakikata tamaa ya kuishi ........

Sababu eti wamechoka?????

Eti umaskini???????

Mahusiano????????!

Bado hujaelewa nini Mungu ameweka ndani yako ndiyo maana unafikia uamuzi huo.

Nikutahadharishe TU kwamba pia utadaiwa kingi na Mungu kwasababu pia ameweka vipawa, karama na Huduma nyingi ndani yako . *Hivyo hakuna muda wa kupoteza fanya kazi*

MWISHO 

Mwanadamu kwa Maarifa Ngu aliyoweka ndani yake ameweza kufanya haya yote yanayoonekana. Nawe amua sasa kutumia kile Mungu amekupatia kuleta mabadiliko duniani.utajiri ni haki yako.

©2023 Mchungaji Johnson Paul Pokeaeli

Alhamisi, 18 Mei 2023

TAMBUA WAKATI WA KUJILIWA KWAKO vol.2

 BWANA ANAJIBU KWA NAMNA USIYODHANI/NJIA ZAKE HAZICHUNGUZIKI

  • usichoke kua na subira/saburi/uvumilivu.
  • Usikate tamaa 
  • Jenga Imani yako Kwa Mungu
  • Linda Amani yako ya moyo wakati wote 
  • Kua na tumani hatakama hitaji lako limekawia kiasi gani



Mfano wa uvumilivu uliojengeka katika Imani Kwa Mungu
  • Ibrahimu alingoja mtoto Kwa muda wa MIAKA Tisini na Kenda NDIPO MUUJIZA wake unatendeka tena katika mazingira ambayo hakutegemea
Tazama uhitaji wa Ibrahimu: kupata mtoto, tena mrithi.

Mwanzo 15:2-4

"[2]Abramu akasema, Ee Bwana MUNGU, utanipa nini, nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki nyumba yangu ni huyu Eliezeri, Mdameski? 

[3]Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa nyumbani mwangu ndiye mrithi wangu. 

[4]Nalo neno la BWANA likamjia likinena, Huyu hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi. "

  • Kuna tofauti Kati ya mtoto na mrithi
  • Mungu anamuahidi Abram kwamba atampatia mrithi Toka Tumbo la mke wake wa ndoa .
Mwanzo 15:4. "Nalo neno la BWANA likamjia likinena, Huyu hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi." 

  • Umri unazidi kwenda na Kwa kigezo hicho Abram anaingia kwenye mtego wa kumkosea Mungu 
  • Shetani anaijaribu Imani yake Kwa kuwadanganya kwamba wanaweza kupata mtoto hata Kwa mjakazi.
  • Wanasahau kwamba wanatafuta mrithi na sio mtoto TU.
Mwanzo 16:1-2
"[1]Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, jina lake Hajiri. 

[2]Sarai akamwambia Abramu, Basi sasa, BWANA amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai. "

  • Kua makini wakati unangojea Baraka zako .
  • Unapongojea MUUJIZA WAKO Adui anaweza kukuletea kila aina ya lugha ,ulagahai Ili kukuyumbisha Imani yako Kwa Mungu usikubali
TENGENEZA NA MUNGU ILI UPOKEE BARAKA ZAKO.
  • MUNGU Anapatiliza maovu yetu hata kizazi baada ya kizazi lakini pia ni mwingi wa rehema akikusamehe atakubariki wewe na kizazi chako chote.
  • Katika wakati wa kungojea ulionao umemkosea nini Mungu : je ulienda Kwa waganga? Au ulizini/ukitoka nje ya ndoa Ii kupata mtoto?
  • Kama ulifanya hivyo inapaswa kutenge eza.
Mwanzo 17:1-3
"1]Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, BWANA akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe m
kamilifu. 

[2]Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana. 

[3]Abramu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema," 

SOMO HILI LINAENDELEA .......
Endelea kufuatilia masomo hayayatakujenga KIROHO nawe utavuka hatua Moja kwenda nyingine. Amen
✍️✍️Mchungaji Johnson Pokeaeli




MBINU ZA KUSHINDA MAJARIBU

 MBINU ZA KUSHINDA MAJARIBU/MITIHANI

1. UTULIVU

2.IMANI KWA MUNGU

3. IMANI KATIKA UWEZO WAKO (Unaweza)

4.KUTHUBUTU KUFANYA PASIPO HOFU NA MASHAKA.




WAKATI UNAKUTANA NA MAJARIBU USISAHAU HAYA:

_________________

1.Shetani ni baba wa uongo

•atakuambia huwezi

•Atajaribu kukuonesha wengine walioshindwa Ili ukate tamaa.

2. Usitafute njia fupi au ya haraka haraka ya kutoka kwenye jaribu hilo.

•Njia ni Yesu Kristo pekee

3. Linda sana Amani ya Moyo, (hali yako ya KIROHO isiathirike Kwa namna yeyote Ile) 

1 Kor 10:13 SUV

"Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili."

Ebr 10:38 SUV

"Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye."

Yakobo 1:5

"Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; *naye atapewa.*"

MAOMBI BILA KUKOMA

1.Hakuna Cha kukufanya usimwombe Mungu,Bali vipo vingi na mambo mengi yanayotufanya twende mbele za Mungu Kwa maombi.


2. Maombi ni Mazungumzo na Mungu wetu

 •je unatambua hilo?

•tumepewa fursa ya pekee sana sana kupeleka mahitaji yetu Kwa Mungu.

•pale hali inapozidi kua ngumu ndiyo na maombi yazidi Kwa wingi Kwa Mungu.

Yakobo 1:6-8

"[6]Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku. 

[7]Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana. 

[8]Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote."

Isaya 62:6 SUV

Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha BWANA, msiwe na kimya

Hitimisho.

Kristo amestuachia uhakika wa kushinda vita yeyote Inayotukabili. MBINU hizi zikuongoze kusimama kikamilifu ktk Imani. 

Endelea kufuatilia masomo yetu . Ahsante

✍️Rev. Johnson Paul Pokeaeli




Jumatatu, 27 Machi 2023

TAMBUA WAKATI WA KUJILIWA KWAKO. WAKATI WA MUUJIZA WAKO

 Mfano wa Mwanamke wa Sarepta,

Katika wakati huohuo ukiwa na njaa Kali NDIPO Bwana anahitaji umtumikie Kwa uaminifu Ili akuinue. Unapimwa Imani yako kwake. Wakati wa Shibe pia usiache kumtumikia 


Wengine wanadhani kutoa sadaka ni Hadi wawe na utajiri mwingi lakini hapana. Embu angalia kisa hiki.

1 Fal 17:8-16 SUV

Neno la BWANA likamjia, kusema, Ondoka, uende Sarepta, ulio mji wa Sidoni, ukae huko. Tazama, nimemwagiza mwanamke mjane wa huko akulishe. Basi, akaondoka, akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni nipate kunywa. Alipokuwa akienda kuleta, akamwita akasema, Niletee, nakuomba, kipande cha mkate mkononi mwako. Naye akasema, Kama BWANA, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili niingie nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe. Eliya akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye kama ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate mdogo ukaniletee; kisha ujifanyie nafsi yako na mwanao. Kwa kuwa BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Lile pipa la unga halitapunguka, wala ile chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile BWANA atakapoleta mvua juu ya nchi. Basi akaenda, akafanya kama alivyosema Eliya; na yeye mwenyewe, na Eliya, na nyumba yake, wakala siku nyingi. Lile pipa la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la BWANA alilolinena kwa kinywa cha Eliya.

Encouraging and challenging you to seek intimacy with God every day.


YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy.